Logo

Bongo Queens! Ni nani 'Leading Lady' wa Mei?

Habari
18 Mei 2018
Tungependa kujua ni ‘Binti wa Kifahari’ au ‘Leading Lady’ wa Maisha Magic Bongo! Piga kura hapa!
MMB ladies feature image

Kutoka kushoto hadi kulia: Tausi, Getrude, Magareth, Aunt Ezekiel na Gladness. 

Ijumaa hii, tunatazama MMBongo Queens! Tulipoanza mwezi wa Mei, waigizaji wetu wa vipindi tuvipendavyo wametuletea burudani ya kipekee! Tungependa kujua ni Binti yupi mashuhuri ungesema ni ‘Leading Lady’ wa Maisha Magic Bongo?

Katika kipindi muhula uliopita wa HARUSI YETU, tulikuwa na shindano la kimataifa! Washindi walipata Harusi ya ndoto zao kwa niaba ya Maisha Magic Bongo na Harusi Yetu! Bibi Harusi, Magareth Richard alitufunza mitindo ya ku-slay, yaani alipendeza sana kwa gauni lake jeusi katika sherehe za ukumbi! Hongera sana Magareth! Mungu aibariki Ndoa yenu! Tunasubiri kwa hamu muhula wa tatu wa Harusi Yetu hivi karibuni!

Kwa mwendo huu, tungependa kujua ni Binti yupi mashuhuri ungesema ni ‘Leading Lady’ wa Maisha Magic Bongo?  Kazi yetu hapa MMBongo ni kuwaletea burudani bila kikomo!

Tausi Mdegela

Wa kwanza ni Tausi Mdegela anayeigiza katika tamthilia ya KAPUNI! Ameleta vichekesho na mada ya kizamani kuhusu ndoa na mahusiano ya kijamii! Tausi ameigiza katika filamu za Bongo kadha wa kadha, na ni msanii mashuhuri hapa Tanzania!

Aunt Ezekiel

Aunt Ezekiel akiigiza katika tamthilia moto moto ya HUBA! Mapambano na muigizaji mwenza Tima kupata penzi la Dev ilileta shamra shamra kali kabisa na kipindi cha HUBA msimu wa pili ulinoga sana! Aunt Ezekiel ni muigizaji maarufu wa filamu na vipindi vya televisheni hapa Tanzania. Tegea msimu wa tatu mwezi ujao!

Gladness Kifaluka

Gladness Kifaluka anaigiza kama Pili katika kipindi cha vichekesho, KITIMTIM! Pili na Zunde ni juha kalulu wa kupindikia na vituko vyao vinavunja mbavu kila tukitazama kipindi hiki! Gladness amekuwa katika sekta ya ucheshi na uigizaji wa filamu kwa miaka mingi! Kina dada wanapaa katika Ulimwengu wa Burudani!

Getrude Muita

Getrude Muita ama ‘Monji’ ni Muigizaji shupavu katika tamthilia mpya hapa MMBongo, REBECA! Ameigiza katika tamthilia nyingi sana, akicheza kama mwanamke anayewarusha wanawake wengine waume wao, na kuishi Maisha ya ki-gangsta!

 Haya basi! Pigeni kura tumjue Leading Lady wa mwezi wa Mei!