Katika msimu mpya wa KiTimTim, mcheshi mashuhuri Haji Salum (Mboto) anatupa buriani za kuonana. Tunaungana na muigizaji na mcheshi hodari, Tin White akiigiza kama Bwana Zunde.
Basi, Tin White ni nani? Martin White ajulikanaye kama “Tin White’ ni msanii alietokea kikundi kikongwe cha Sanaa KAOLE GROUP. Ameshawahi kucheza movie nyingi na tamthilia mbali mbali zikiwemo ENGLISH COURSE, SONGOMBINGO, NYUMBA YA KUPANGA, PIKIPIKI na nyinginezo nyingi.
Kwa sasa, Tin white anazidi kungara na kipaji chake kwenye Vichekesho vya Kitimtim kama mume wa Pili aliyeigizwa na Gladness Kifaluka.
KiTimTim ni simulizi kuhusu mwanaume mwenye wanawake wengi, amejaa na visa na uongo mwingi. Zunde anaipenda familia yake na ni mwanaume anaependa watoto ijapokua hajafanikiwa kupata watoto. Mke wake Pili anaamua kwenda bega kwa bega akipambana na wanawake wa mume wake!
Kupata uhondo Zaidi na matangaza kuhusu KiTimTim, fuata kurasa zetu za kijamii, @maishamagicbongo
Kipindi kinawajia kila Jumatatu saa 1;30 Usiku katika Maisha Magic Bongo Pekee! Usikose!