Logo

Tin Martin ni Zunde katika Kitimtim!

Habari
13 Aprili 2018
Haji Salum anampa nafasi Tin Martin katika kipindi cha KiTimTim! Pata taarifa hapa!
<p>Kitimtim cover</p>

Katika msimu mpya wa KiTimTim,  mcheshi mashuhuri Haji Salum (Mboto) anatupa buriani za kuonana. Tunaungana na muigizaji na mcheshi hodari, Tin White akiigiza kama Bwana Zunde.


Basi, Tin White ni nani? Martin White ajulikanaye kama “Tin White’  ni msanii alietokea kikundi kikongwe cha Sanaa KAOLE GROUP. Ameshawahi kucheza movie nyingi na tamthilia mbali mbali zikiwemo ENGLISH COURSE, SONGOMBINGO, NYUMBA YA KUPANGA, PIKIPIKI na nyinginezo nyingi.

Kwa sasa, Tin white anazidi kungara na kipaji chake kwenye Vichekesho vya  Kitimtim kama mume wa Pili aliyeigizwa na Gladness Kifaluka.

KiTimTim ni simulizi kuhusu mwanaume mwenye wanawake wengi, amejaa na visa na uongo mwingi. Zunde anaipenda familia yake na ni mwanaume anaependa watoto ijapokua hajafanikiwa kupata watoto.  Mke wake Pili anaamua kwenda bega kwa bega akipambana na wanawake wa mume wake!

Kupata uhondo Zaidi na matangaza kuhusu KiTimTim, fuata kurasa zetu za kijamii, @maishamagicbongo

Kipindi kinawajia kila Jumatatu saa 1;30 Usiku  katika Maisha Magic Bongo Pekee! Usikose!